Monday, November 28, 2016

WIZARA YA ELIMU JANA IMETOA TAMKO RASIMI KUPTIA KWA WAZIRI WA ELIM JOYCE NDALICHAKO

Profesa Joyce Ndalichako
Mara hii, ikiwa yaliyomo katika Hotuba yake yatatekelezwa, utakuwa mwisho wa moja ya mifumo iliyokuwepo ambapo mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne angeweza kuamua kusoma ngazi ya Diploma yaani Stashahada badala ya kupitia katika ngazi ya kidato cha sita.
Waziri huyo wa Elimu anaongeza kuwa wanafunzi wasiofaulu katika kidato cha nne wamekuwa wakienda kusoma ngazi ya cheti, kisha Stashahada na baadaye wakipenya na kuelekea katika Shahada yaani digrii lakini sasa watalazimika kupitia katika ngazi ya kidato cha sita.
Ambao hawatapitia katika safari ya kidato cha sita ni wale watakaofaulu katika kidato cha nne na kuchaguliwa kwenda kusoma katika vyuo vya ufundi daraja la kati.
Mfumo mwingine pia utakaaoathirika ni ule ambao mwanafunzi aliyehitimu kidato cha sita lakini akashindwa kukamilisha vigezo kadhaa vinavyotakiwa katika vyuo vikuu alikuwa anapata nafasi ya kufanya masomo ya muda yaani 'Foundation Course' katika Chuo kikuu huria cha Tanzania na kama angefaulu angeruhusiwa kuendelea na masomo ngazi ya degree.

No comments:

Post a Comment